0
Jacqueline Wolper alipewa jina la utani ‘Wolperstylist’ na mashabiki kutokana na jinsi anavyotupia pamba kali.
Tumezungumza na mrembo huyo kutaka kujua mapenzi yake kwenye fashion na kama anapata changamoto kuhakikisha anapendeza muda wote.

“Ni hobby sana sana, hakuna challenge kwasababu kila mtu anapenda kitu chake,” amesema Wolper. “Mimi napenda kuvaa.”

Katika hatua nyingine Wolper amesema ameshafikiria kuja na kipindi cha TV cha masuala ya fashion lakini anahitaji kujifunza zaidi.

“Movie ni kazi yangu ambacho ni kipaji changu lakini hivyo vingine nina idea navyo kidogo tu na kuna watu ambao tayari wameshaingia kwahiyo vitu vingine mpaka nijifunze labda ndio niingie.”

Wolper pia alisema bado amesimama kufanya filamu kutokana na sababu mbalimbali.

Post a Comment

 
Top