0
Kundi la Weusi usiku wa kuamkia leo limerekodi wimbo na rapper wa Afrika Kusini, Kiernan Jordan Forbes maarufu kama AKA.
Rapper huyo yupo nchini kwaajili ya kuhudhuria ‘Zari All-White Party’ iliyofanyika Ijumaa hii Mlimani City.

Joh Makini, Nick wa Pili na G-Nako pamoja na AKA waliungana na producer Tuddy Thomas kwenye session ya usiku huku beat ya collabo hiyo ikifanywa na Nahreel.

“TOKA STUDIO NOW….ITS DONE WEUSI FT AKA….BIG S/O @diamondplatnumz…KWA KUMLETA AKA TZ..BILA WEWE HII COLABO ISINGEWEZEKANA …S/O @adamchomvu BABA LA BABA…S/O @nahreel ON THE BIT..@tuddthomas on the session,” ameandika Nick wa Pili kwenye Instagram.

Post a Comment

 
Top