0

Nimeona kukaa kimya sio dawa. Nasikitishwa sana na watu wanaosema kwamba mimi nipo upande wa Alikiba na namponda Diamond, kitu ambacho hakina ukweli wowote.

 Ifahamike kwamba hawa wote ni madogo zangu na wote nawakubali kwa mchango wao na kuleta chachu katika gemu la muziki wa Bongo. 

Ieleweke kwamba Sina bifu na yeyote kati yao, kuposti picha nikiwa na mmoja wao haina maana nipo team flan au nipo upande wa mmoja wao. Kama wewe ni mpenda AMANI na ungependa siku hawa watu wamalize tofauti zao, fanya kuComment 'Peace'. Ndio nshamaliza hivyooo sihitaji tena maswali mengine kuhusu wao. Ovaaaaaaaaaaaa hayo ndio maneno ya juma nature kupitia official account yake ya facebook..

Post a Comment

 
Top