0
Muimbaji wa ‘Chekecha’, Alikiba amesema kwa sasa hafanyi tena muziki wa playback bali ni live peke yake.
Akiongea na 255 ya XXL kupitia kituo cha redio cha Clouds FM, Kiba alisema siku si nyingi ataitambulisha bendi yake.

“Nimeamua kuacha kufanya muziki wa playback, na sio muda mrefu wataniona na bendi yangu na nimeshafanya mipango hiyo tayari bado tu kuitangaza,” alisema.

“Burudani ya show yangu yoyote ya Kiba itakuwa ni live band labda itokee tu bahati mbaya hiyo sehemu band haiwezekani. Kingine ukifanya na bendi unakuwa na uchungu zaidi na hela yako na kingine unakuwa serious zaidi yale sijui mambo ya mikono juu kidogo yanapungua.”

Post a Comment

 
Top