0
Kundi la Kwaito la nchini Afrika Kusini, Big Nuz limelazimika kusitisha show yao iliyokuwa ifanyike jana mjini Bulawayo, Zimbabwe ili kujikita katika jitihada za kumaliza mashambulio dhidi ya raia wa kigeni kwenye jimbo la KwaZulu Natal.
Kwa mujibu wa gazeti la serikali la Zimbabwe, The Herald, kundi hilo limekuwa likipokea vitisho kutoka kwa rais wa Zimbabwe.

Big Nuz si wasanii pekee wa nchi hiyo waliopokea vitisho kupitia mitandao ya kijamii.

Rapper Cassper Nyovest naye alitishiwa maisha yake ikiwa anajiandaa kwa ziara yake ya Zimbabwe April 25.

Post a Comment

 
Top