0
Msanii wa muziki wa asili, Mrisho Mpoto amejikuta mpweke baada ya kupuliziwa dawa na wezi na kuibiwa vitu vya ndani vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 7 usiku wa kuamkia leo.
Akizungumza na Bongo5 kwa masikitiko, Mpoto amesema wezi hao huenda waliwapulizia dawa hali ambayo ilisababisha kutoshtukia mchezo huo.

Sehemu ya TV na radio

“Yaani wamesafisha kila kitu,” amesema Mpoto. “Hapa sebuleni hakuna kitu yaani. Mimi mwenyewe nilikuwepo sema labda ni kwa sababu nyumba kubwa pia tunahisi labda walitumia dawa kwa sababu sio kawada nikalala hivyo bila kusikia kinachoendelea. Nahisi walitupulizia dawa za usingizi. Pesa nyingi sana ni zaidi ya milioni 7, sema tayari suala nimelifikisha polisi na wanaendelea na upelelezi. Wameiba vitu ni vingi, flati screen, maredio yaani ni vingi.”

Post a Comment

 
Top