0
Msanii wa filamu, Wastara Juma amenusurika kifo baada ya kupata ajali ya gari. Hiyo ni ajali yake ya 9 kuwahi kupata.
Wastara amewahi kupata ajali ya gari iliyomlazimu akatwe mguu wake.

“Dua zenu muhimu sana kwa mbao mnaonipenda na msionipenda,” ameandika kwenye picha aliyoweka Instagram inayomuonesha akiwa na jeraha usoni.

“Hali hii imenichosha sana ya matukio ya ajali kila mara natamani kuwa na amani na maisha yangu couz mungu ana sababu kuniacha niendelee kupumua mpka leo ila kwa wanaochukia kuona napumua wanatamani nizikwe hta mzima ila mtambue nina watot 3 wananitegemea kwa kila kitu smtime mnasema nasikitika sana ni kweli sababu mi sio nabii,” aliongeza.

“Nikihesabu hii ni ajali ya ya 9 sasa tena ni mbaya sana za kufa kabsa ila labda nimo kwa wale wanaopta ajali kipindi hiki japo kwangu ni too much,, ni jana na leo napumua alhamdulilah duwa zenu niombeni jamani huyu jinamizi akae mbali nami daah too much.”

Post a Comment

 
Top