0
Rapa mwenye sauti nzito Jeffrey Atkins, maarufu kama Ja Rule ameweka wazi muelekeo wa kura yake kwenye uchaguzi ujao wa rais nchini Marekani na kusema atampigia Bi Hillary Clinton. Mwandishi Melissa Francis wa kipindi cha Tv cha Fox Business’s Money kutoka nchini Marekani, alimuuliza Ja Rure ni nani angependa awe Rais wa Marekani 2016?.

” Ningependa sana Hillary Clinton najua mambo yanachanganya sababu hata Jeb ni mgombea mzuri, lakini nitampigia kura Clinton”, alijibu Ja Rule.

Bi Clinton ni Mwanamke pekee alijitokeza kugombea nafasi ya urais wa nchini Marekani kwenye uchaguz mkuu utakao fanyika mwakani.

Post a Comment

 
Top