0
Muimbaji kutoka mji kasoro bahari Morogoro, Belle 9 anategemea kukata kiu ya mashabiki wake kwa kuachia wimbo mpya uanaoitwa ‘Shaurizao’ Ijumaa hii (March 27).
Belle 9 amesema kuwa kitu cha tofauti kwenye wimbo huu ni kuwa utakuwa na ladha tofauti na iliyozoeleka kwenye nyimbo zake sababu amefanya na production tofauti.

“kipya ni production tofauti na watu walivyozoea, nimefanya pale Kiri Records chini ya Rush don. Niliikuta beat pale jamaa akaniskilizisha beat tukaimodify kidogo nikaichukua nikaenda kuiandikia verse na chorus halafu verse ya pili nikaifanyia studio”.

Kuhusu mipango ya video ya wimbo huo Belle 9 amesema kuwa itategemea na wimbo utakavyopokelewa, lakini upo uwezekano wa kufanya video ya wimbo mwingine sababu ana nyimbo nyingi hivyo itakuwa surprise.

Mwezi uliopita Belle 9 alitoa video ya wimbo aliomshirikisha Joh makini ‘Vitamin Music’ ambayo iliongozwa na Khalfani.

Post a Comment

 
Top