0

Huenda watu wanamfahamu Floyd Mayweather sio kwa sababu labda kila mtu anapenda mchezo wa Boxing.. au kila mtu anampenda, kiukweli wako wanaomfahamu kwa sababu ya mbwembwe zake, vioja vyake kwenye media, au labda watu wanamfahamu kwa sababu ni mwanamichezo ambaye analipwa pesa nyingi zaidi duniani kwa sasa!

Tunaisubiri May 2 2015, kila kilichosemwa itakuwa ndio mwisho wake kuhusu nani mbabe kati ya Mayweather na Manny Pacquiao, huku vichwa vya habari Magazetini duniani na mitandaoni vikiwa na story nyingi sana kuhusu wao tangu siku ya kwanza jamaa walipotia saini kwamba YES watapigana.

Nikusogezee kingine cha Floyd mtu wangu.. taarifa kuhusu yeye kwa leo ni juu ya kiasi cha pesa ambacho jamaa anakitoa kwa ajili ya chakula tu, yani ile diet yake mpaka siku ambayo watakuwa ulingoni na Manny.

Dola 4,000 kwa siku ndio kiasi ambacho Floyd atakuwa akilipa kwa siku kwa ajili ya chakula tu, na hesabu iliyofanywa ni kwamba mpaka May 2 atakuwa ametoa Dola 184,000, kwa Bongo ni kama Mil.330/= kwa ajili ya chakula ambacho kinaandaliwa na mpishi wake Chief Q.



Kwa hesabu zetu ni kiasi kikubwa sana cha pesa, mwingine anaona ni kama mtaji wa biashara kubwa ambayo anawaza labda kuifanya, lakini Chief anasema hicho ni kiasi kidogo sana cha pesa kwa uwezo wa Floyd, haimpi shida kuilipa.

Moja ya vitu ambavyo wanamichezo wanashauriwa sana kujali ni ishu ya mpangilio mzuri wa chakula, Floyd anaangalia hilo pia na sio gharama za yeye kupata huduma hiyo mtu wangu.

Mfano unapata wewe hilo fungu la Dola 184,000/= unaweza kufanyia nini mtu wangu? Nitafurahi kuona comment yako..

Post a Comment

 
Top