Mwimbaji nyota wa Jahazi Modern Taarab Fatma Mohamoud maarufu kama Fatma Mcharuko au Fatma Nyoro, Alhamisi iliyopita alikwaa jukwaa la Mashauzi Classic ndani ya ukumbi wa Mango Garden Kinondoni.
Katika kile kinachoonyesha wazi kuwa makundi hayo mawili ya taarab yenye mashabiki wengi zaidi hayana bifu, mkurugenzi wa Mashauzi Classic akampandisha jukwaani Fatma Mcharuko ili kuwasabahi mashabiki na kuwapa ladha kidogo ya ngoma za Jahazi.
Fatma Mcharuko akaimba kipande cha wimbo wake “Aso Kasoro” ambao ulipagawisha ukumbi mzima.
Lakini mashabiki wakapagawa zaidi pale mwimbaji huyo alipokumbusha juu ya onyesho la Jahazi na Mashauzi Classic litakalofanyika Jumapili ya tarehe 22 mwezi huu kwenye ukumbi wa Travertine ambapo akasema si mpambano ila kufunikana imo …mashabiki wakalipuka kwa furaha.
Baadhi ya watu wengine wa Jahazi waliokuwepo ndani ya ukumbi wa Mango Garden ni mkurugenzi msaidizi Hamis Boha na mpiga solo Emeraa ambaye nae pia alipanda jukwaani kupiga wimbo wa “Aso Kasoro”.
Isha akimtambulisha Fatma Mcharuko
Fatma Mcharuko akichekwa kwa maneno ya Isha
Fatma Mcharuko akiongea machache
Emeraa Solo wa Jahazi akimpigia gitaa Fatma Mcharuko
Mcharuko akipandisha watu mzuka
Mashabiki wakipagawa na uimbaji wa Mcharuko
Fatma Mcharuko akimkumbatia Isha kwa furaha mara baada ya kumaliza kuimba
Hapa akipozi na Zubeida Malick
Mkurugenzi msaidizi wa Jahazi Hamis Boha akipozi na Isha Mashauzi
Hapa Fatma Mcharuko anacheza goma la Mashauzi
Home
»
Bongo star
»
STORY
»
TeamKaziEntertainment
» PICHA 10: FATMA MCHARUKO WA JAHAZI KWENDA MASHAUZI CLASSIC MANGO GARDEN …
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment