0
Alikiba ameanza kupenya katika vituo vya radio vya Nigeria.
Wimbo wake ‘Chekecha Cheketua’ umeingia kwenye ‘African Top 10′ ya Radio kubwa iitwayo The Beat 99.9 Fm iliyoko Lagos, Nigeria ukiwa umekamata nafasi ya 9 wiki hii.

Msanii mwingine wa Tanzania ambaye yuko kwenye chart hiyo ni Diamond Platnumz, wimbo wake ‘Nana’ aliomshirikisha Flavour umekamata nafasi ya 2 wiki hii.

Hao si wasanii pekee wa Afrika Mashariki ambao nyimbo zao ziko kwenye chart, kutoka Uganda Jose Chameleone anawakilisha kupitia wimbo aliomshirikisha na Patoranking wa Nigeria ‘Only You’ ambao umekamata nafasi ya 7, huku Maurice Kirya na wimbo wake wa ‘Never Been In Love Before’ umekaa katika nafasi ya 5.

Post a Comment

 
Top