0
Tetemesha Entertainment inamtambulisha msanii mpya kutoka Rock City, aitwaye - COYO. Huyu atakuwa ndio msanii wa kwanza anaye Rap kufanya kazi na Tetemesha baada ya Hussein Machozi, Sajna na Barakah Da Prince.

NOMA, ndio jina la wimbo rasmi unaomtambulisha COYO ambao umerekodiwa jijini Mwanza chini ya producer mkali na mwenye dalili za kuja kusumbua kwa kazi kali aitwaye Day Dream.

Moja ya utambulisho ambao COYO alioamua kuutumia katika kazi zake, ni pamoja na kuchanganya maneno ya Kisukuma kwenye nyimbo zake.

“Nimeamua kuchanganya Kisukuma kwenye wimbo wangu maana mimi ni msukuma, na pia napenda kuonesha uzalendo kuanzia kwenye utunzi kama Mtanzania halisi ninaye jivunia asili yangu, na pia nataka iwe moja ya utambulisho wangu wa kunitofautisha na wengine” amesema COYO .

Hii ni baadhi ya mistari aliyochanganya na Kisukuma pamoja na tafsiri zake:

Pesa Shane shone  (pesa zangu zote )/
Nakwine unine nami npone  (nikupe unipe na mi nipone )/
Nyonga mpaka nikome /
Nakutoole (nikuoe)/
Nkutwale(nikupeleke)/
Kokaya kome   (nyumbani kome )/”

Licha ya kuwa na kipaji cha kuandika na kurap, COYO pia ana kipaji cha kuimba kama alivyofanya kwenye chorus ya wimbo huu.
Tizama video,sikiliza audio na kudowload

Post a Comment

 
Top