0
Matatizo hayaishi kumwandama Tyga. Rapper huyo anashtakiwa na mtu aitwaye Alex Benedict, anayedai kuwa ameshindwa kulipa deni analodaiwa baada ya kukodi Ferrari 488.
Kwa mujibu wa nyaraka za kisheria, Tyga aliacha kulipa fedha hizo kufuatia mkataba alioingia mwezi May.

Gari hilo limewahi kuchukuliwa mara mbili. Mara ya kwanza, gari lake lilichukuliwa August lakini Tyga alilichukua tena na kupangwa kulirejesha Oct. 9. Benedict anadai kuwa rapper huyo alishindwa kufuata makubaliano na gari likachukuliwa tena Nov. 8.

Benedict sasa anamshtaki T-Raww akitaka alipwe $150,000 kutokana a hasara aliyopata.

Post a Comment

 
Top