Hata hivyo uongozi wa Diamond umedai kuwa barua hiyo nao wameiona kupitia mtandaoni lakini haijawafikia mkononi.
“Tunasikia tu kwenye mitandao hatuna taarifa nayo, maana hawajawasiliana na sisi,” amesema Salam, mmoja wa mameneja wa Diamond Platnumz.
“Inashangaza kuona kitu kwenye mitandao bila ya kuambiwa mhusika mkuu, tumechukulia kama changamoto zilizopo kwenye maisha,” ameongeza.
Diamond bado yupo nchini Nigeria alikoenda kutumbuiza kwenye ‘The Africa Magic Viewers’ Choice Awards 2015’.
Diamond akiwa kwenye selfie ya pamoja na mastaa mbalimbali wa Nigeria akiwemo 2 Face, Iyanya, Paul Okoye na wengine
Post a Comment