0
Mshambuliaji wa Yanga, Mrisho Ngassa jana April 21 katika mechi dhidi ya Stand United iliyochezwa kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam alifunga goli moja lakini hakushangilia kwa kawaida yake ya kwenda kwenye kona ya kibendera, bali alionekana akibusu mkono wake.
Ngassa aliongea na kipindi cha Sports Xtra cha Clouds FM na kueleza kwanini aliubusu mkono wake.

“Nimebusu mkono kwasabababu nimechora ‘Tattoo’ ya jina la mke wangu. Mke wangu ndio kila kitu, ndio mshauri wangu wa kila kitu, kwahiyo nikifunga goli lazima nimbusu,” alisema.

“Tattoo niliyochora ni jina la mke wangu kwasababu nina mapenzi ya dhati kwake, yeye ndiye mshauri wangu, anaitwa Nish Radhia. Kuna tattoo nyingine ambayo ni siri yangu pamoja na yeye, imechorwa kifuani.”

Post a Comment

 
Top