“Nakubaliana na wewe Tip Top ya enzi zile za tunapanda ilikuwa kama timu ya taifa vile, maana umoja ulikuwepo na wala hakukuwa na majungu yani kila mmoja alisimamia nafasi yake” alisema Tunda.
Pia Tunda Man alisema anatamani Cassim Mganga arudi tena kundini Tip Top kutokana na uwezo wake pamoja na sauti yake.
“Kiukweli Cassim natamani arudi yani kwakuwa bado hatujampata mbadala wake, unajua sauti yangu na yake(Cassim) zilikuwa zinaendana sana na Madee akipita na bass basi inakuwa poa sana, kwa kweli hakuna aliyeziba pengo lake” alimaliza
Tunda ameenda mbali zaidi kwa kusema baada ya kuondoka kwa Cassim Mganga, Tip Top imeyumba.
Post a Comment