Kwa mujibu wa vyanzo, Jay Z bado hajakamilisha makubaliano ya mkataba na Sony ambao wanataka walipwe kiasi kikubwa cha fedha kama kianzio kwaajili ya kutoa haki za kuwekwa kwa nyimbo zao.
Universal na Warner tayari wameshamaliza makubaliano na Tidal.
Kama Jay Z atashindwa kuwalipa Sony fedha wanayoitaka, Bloomberg imesema nyimbo za wasanii wake wengine wakiwemo Daft Punk, Alicia Keys, na Usher zitaondolewa kwenye Tidal.
Hivi karibuni Sony ilifuta nyimbo zake kutoka kwenye mtandao wa SoundCloud kwa sababu hizo hizo. Hata hivyo Bloomberg imedai kuwa Tidal iko vizuri kifedha na hivyo hili linaweza kuwa ni suala dogo.
Post a Comment