“Bado tuko kwenye mazungumzo ya mwisho na tumeshatumiana nyimbo, ameomba maelekezo, na ameridhia lakini sasa hivi kumtaja kidogo nimeambiwa nisubiri, lakini yeye ameonyesha interest ya kutaka kufanya huo wimbo na ameupenda ameomba atumiwe mashairi atumiwe beat, kwahiyo kuna uwezekano ikawa na mafanikio.” alisema Ben Pol.
Hit maker huyo wa ‘Sofia’ ameongeza kuwa licha ya kuwa anamshirikisha msanii wa Nigeria lakini wimbo huo utakuwa na mahadhi ya R&B kama ambavyo amekuwa akifanya kwenye nyimbo zake.
Kama mipango ikifanikiwa basi hiyo ndio itakuwa collabo ya kwanza kubwa kwa Ben Pol kufanya na msanii wa kimataifa.
Post a Comment