0
Tuzo za Brit awards 2015 zimefanyika jana usiku kwenye ukumbi wa O2 Arena, London huku mastaa mbalimbali kama akina Taylor Swift, Kanye West na Madonna.
Ushindi wa akina Sam Smith na wengineo kupata tuzo huenda isiwe story kubwa kwa leo, tukio la kuanguka kwa mwanamuziki mkongwe Madonna limezungumziwa zaidi, hii imetokea bahati mbaya wakati mwanamama huyo akifanya show na dancers wake kwenye stage.
Tukio la kuanguka halikuathiri kitu kwenye show ya mama huyo, aliinuka na kuendelea kufanya show yake. 

Baadaye staa huyo ambaye ana umri wa miaka 56 aliandika ujumbe wa mashabiki wake kupitia Instagram kuwa hali yuko poa na ajali aliyoipata kwenye stage ilikuwa ni bahati mbaya, kwenye video inaonyesha alikuwa amevaa nguo ndefu ambayo huenda ilikuwa ivutwe ili aivue wakati akiwa anapanda ngazi lakini nguo hiyo ilikuwa imekazwa sana shingoni hivyo haikuvuka kirahisi kama walivyopanga.




Armani hooked me up! My beautiful cape was tied too tight! But nothing can stop me and love really lifted me up! Thanks for your good wishes! I’m fine! ❤️#livingforlove

A photo posted by Madonna (@madonna) on Feb 25, 2015 at 2:50pm PST

Post a Comment

 
Top