0
Kundi lililotajwa kuwania tuzo za MTV MAMA mwaka huu, Navy Kenzo, litaachia album yake mpya ‘Above In a Minute’ December mwaka huu.
Taarifa hizo zimethibitishwa na member na producer wa kundi hilo, Navy Kenzo kupitia Instagram. “THE WAIT IS OVER #Aim i cant wait for the world to listen to this Album #ComingOutThisDecember,” ameandika Nahreel.

Kwa muda mrefu Navy Kenzo walikuwa wakiiandaa album hiyo itakayowashirisha wasanii mbalimbali ndani na nje ya Tanzania.

Hivi karibuni walidai kuwa watakuja na wimbo mkubwa zaidi kutoka kwenye album hiyo unaoweza kuwapeleka katika hatua kubwa zaidi kimuziki.

“Tumekuwa tukifanya muziki mzuri na wa tofauti ili tuifikishe Bongo Flava mbali. Sasa kuna nyimbo inakuja watu wakae tayari kwa sababu tumewekeza sana kwenye production na kila kitu,” waliiambia XXL ya Clouds FM.

“Ni ngoma kali sana kuanzia style na kila kitu. Pia album yetu ‘Above In a Minute’ inakuja na wnyimbo hiyo itakuwepo pia, tunataka tufanye vitu vikubwa ikiwemo kuzifikia chati za Billboard,” waliongeza.

Post a Comment

 
Top