0
Rapper Fareed Kubanda aka Fid Q amedai kuwa kampeni aliyoanzisha mwaka jana ya Tu8 January ambayo ilishuhudia kufanyika kwa ziara za wasanii katika baadhi ya maeneo nchini, haina uhusiano wowote na January Makamba.
Akiongea kwenye kipindi cha Mambo Mseto cha Radio Citizen ya Kenya, Fid alisema kampeni hiyo ilijihusisha na kuwataka vijana kujitokeza kwenda kujiandikisha kupiga kura na kujitokeza kwaajili ya kugombea nafasi za uongozi.

“Ni kwasababu Tanzania tulipofanya sensa juzi kati hapa ikaonekana kabisa kwamba 80 percent ya watanzania ni vijana. Kwahiyo huwa tuna msemo wetu vijana ni taifa la kesho lakini sasa umekuwa sio tena taifa la kesho, ni taifa la sasa so the future is now,” alisema.

“Nani wa kuweza kutusaidia sisi the majority? Ni vijana wenzetu ambao wanajua matatizo yetu, so my idea ni kwenda kuwaamsha vijana.”

Post a Comment

 
Top