0
Msanii Dezert Eagle ambaye makazi yake yapo nchini Australia ambako mwaka jana alishinda tuzo ya za AAMA za nchini kwa wimbo aliomshirikisha Diamond Platinumz, amerejea Tanzania kufanya collabo nyingine.
“Nimekuja Bongo kufanya kazi nyingine na wasanii wa huku pamoja na kushoot video,” msanii huyo ameiambia Bongo5.

“Pia mwanzo nilifanya collabo na Diamond Platnumz na huo wimbo ulipata tuzo kule Australia. Nilifanya pia wimbo na Linah, video pia nilishoot hapa hapa. Sasa hivi nimekuja kufanya kazi na wasanii wa Bongo. Napenda sana kufanya kazi na wasanii wa bongo najua kule hamna mziki kama huu, kwahiyo inakuwa rahisi pia kuutangaza muziki wa bongo pamoja na wasanii wa huku kupata nafasi kule. Pia napata ladha tofauti,” ameongeza.

Dezert amesema amekuja na tuzo zake kuwaonyesha Watanzania yale aliyoyaita ‘matunda ya kazi za nyumbani.’

Post a Comment

 
Top