0
Mwanzilishi wa style iliyokufa ya ‘Takeu’ Lucas Mkenda a.k.a Mr Nice, amewabeza wasanii wanaong’ang’ania kusuburi show za Dar es salaam na kudai amegundua pesa za wasanii zipo mikoani.
Mr Nice ameiambia Bongo5 kuwa wasanii waache kung’ang’ania jiji la Dar na wajaribu kuzunguka mkoani.

“Dar hamnioni sasa,” amesema muimbaji huyo. “Maisha yangu ni mikoani tu huku ndo pesa za wasanii ziliko. Nimegundua wasanii wengi wanang’ang’aniA kukaa Dar Halafu hawana kitu. Wazunguke mikoani huku pesa zipo. Mimi nafanya show nafanya show mpaka katikati ya wiki.”

Post a Comment

 
Top