0
Tangu atoe wimbo wake ‘Nasema Nawe’, Diamond Platnumz anaonekana kukubalika sana kwenye jumuiya ya wanamuziki wa Taarab na Mduara nchini.
Baada ya kumshirikisha Malkia wa Mipasho, Khadija Kopa, huenda Diamond akasikika tena kwenye wimbo wa Mzee Yusuf.

Akiongea kwenye kipindi cha Ng’ari Ng’ari cha Clouds TV, Mzee Yusuf alisema huenda akamshirikisha Diamond kwenye wimbo uitwao ‘Kikulacho’.

Katika hatua nyingine, Mzee Yusuf alisema nyimbo zake zitakazokuwepo kwenye album yake ijayo zitakuwa na si zaidi ya dakika 5.

Post a Comment

 
Top