0
Muimbaji wa ‘Nyota’, Peter Msechu amesema project yake na Baba Levo iitwayo ‘Tumbili wa Town’ bado ipo pale pale.
Akiongea na 255 kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM, Msechu alisema kwa sasa wamesimamisha kidogo kutokana na kuweka mipango sawa huku kila mmoja akiendelea kufanya mambo yake japo hiyo haimaanishi kuwa wameachana na mpango wao.

Katika hatua nyingine Msechu alisema tokea ametoa wimbo wake ‘Nyota’ aliomshirikisha Amini amekuwa akipata show nyingi za live zinazomuingizia kipato kikubwa.

Post a Comment

 
Top