0
Walisema ndoa yao haitodumu, lakini Kanye West na Kim Kardashian wamewaprove wrong waombea mabaya.
May 24, wawili hao watatimiza mwaka mmoja wa ndoa iliyofungwa nchini Italia. Na katika kusherehekea mwaka mmoja wa ndoa, wawili hao wanatarajia kurudia tena viapo vyao.

Dr. Kanye West, 37 na Kim, 34 watafanyia shughuli hiyo kwenye mnara maarufu wa Eiffel jijini Paris, kwa mujibu wa UsWeekly.


Mnara wa Eiffel

Kanye anadaiwa kupanga kufanya kitu kikubwa kwaajili yao. Rapper huyo atakodi mnara huo ambako familia yao itawasaidia kusherehekea.


North West, mtoto wao wa pekee

Mama yake Kim, Kris Jenner, 59 na dada zake, Kourtney, 36, Khloe, 30, Kendall Jenner, 19 na Kylie, 17 watakuwepo.

Pia kamera za Keeping Up With The Kardashians nazo zitakuwepo.

Post a Comment

 
Top