0
Chris Brown amevichana vyombo vya habari vya Marekani kwa kupuuzia mradi wa Akon wa kusambaza umeme wa jua kwa waafrika milioni 600 na kuandika masuala mengine yasiyokuwa na faida.
Ametolea mfano jinsi ambavyo habari ya Bruce Jenner kujibadilisha kuwa mwanamke ilivyochukuliwa kwa uzito kuliko mradi wa Akon.



Hata hivyo kauli hiyo ambayo aliisema kwenye mtandao wa Instagram imemletea matatizo kutoka kwa watoto wa Bruce, Kyle na Kendall Jenner.



Kyle alicomment kwenye picha hiyo aliyoiweka Chris Brown na kuandika: Not very nice to say about your friend’s dad.”

“State what you want about the world without bashing others. Leave a positive impact,” aliandik tena Kyle kwenye Twitter.

Chris Brown ameifuta picha hiyo.

Post a Comment

 
Top