0
Mkurugenzi wa Mkubwa na Wanawe, Said Fella amesema wasanii wa kundi la Yamoto Band wanaruhusiwa kufanya kazi zao binafsi.
Fella ameiambia Clouds FM kuwa hilo sio jambo jipya kwakuwa hata Aslay alianza kama msanii anayejitegemea.

“Hatuwezi kuwakatalia hao kisa wapo kwenye bendi. Si kuna watu wapo kwenye mabendi lakini wanafanya nyimbo zao za solo kwahiyo kwetu hakuna kipingazi hicho,” alisema Fella.

Post a Comment

 
Top