0
Kwa picha zake za Instagram, inaonekana asilimia 70 ya maisha ya Agnes Masogange huyatumia akiwa nje ya Tanzania.
Kwa muda mrefu amekuwa akiishi Afrika Kusini ambako huenda hukutana na mastaa wengi wanaoishia kupagawa na umbo lake!



Kama si kumwona kama ‘mwanaume wa ndoto yake’, kuna dalili kuwa huenda mrembo huyo akawa na uhusiano na msanii na producer wa Nigeria, Tekno Miles.


Tekno Miles

Ukiangalia ukurasa wake wa Instagram utaona kwenye picha yake ya profile ameweka picha ya Tekno Miles lakini pia jina lake amelibadilisha kuwa ‘Didimiles’ hivyo kuna uwezekano mkubwa wawili hao wakawa ‘item’.

Siku wakiamua kuuweka wazi uhusiano wao tutajua!

Tekno Miles ni msanii aliyepewa jina la Chris Brown wa Nigeria kutokana na uimbaji wao kufanana na alizaliwa kwa jina la Augustin Miles.

Post a Comment

 
Top